Monday, July 17, 2017

WAWKLI WAFA MAJI WAKATI WAKIBATIZWA, JESHJ LA POLISI LAMTIA MBALONI MCHUNGAJI

Watu wawili wamefariki dunia kwa  kuzama katika mto Ungwasi wakati wakiwa kwenye ibada ya ubatizo.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro, linawashikilia watu watatu akiwamo mchungaji wa Kanisa la Siloamu wilayani Rombo kwa uchunguzi kwa madai kuwa waumini hao walizama wakati wakiwa katika ibada iliyoandaliwa na kanisa hilo.

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Hamis Issah amesema tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana, kwenye mto Ungwasi uliopo Kijiji cha Keni Kata ya Manda chini wilayani hapa.

Issah amewataja waliofariki dunia kuwa ni Gasper Utoh (47) na Proches Mrema (30).

Kamanda amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Huruma kwa uchunguzi zaidi.

Akielezea tukio hilo, Mkuu wa wilaya hiyo Agness Hokororo amesema waumini hao walifariki dunia wakati wakibatizwa.

Sunday, July 16, 2017

Rais Magufuli Ampa pole mwakyembe

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison George Mwakyembe kufuatia kifo cha mkewe Bi. Linah George Mwakyembe kilichotokea usiku wa tarehe 15 Julai, 2017.

Bi. Linah George Mwakyembe amefariki dunia katika hospitali ya Agha Khan Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Katika salamu hizo, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kushtushwa na kusikitishwa na kifo hicho, na amesema yeye na familia yake wanaungana na familia ya Dkt. Mwakyembe katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

“Nakupa pole sana Dkt. Mwakyembe kwa kuondokewa na mkeo mpendwa Bi. Linah, natambua hisia za maumivu ulizonazo wewe na familia nzima, nyote nawaombea Mwenyezi Mungu awatie nguvu, awape subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

"Namuombea Marehemu Linah George Mwakyembe apumzishwe mahali pema peponi, Amina” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Waziri KASIM MAJALIWA Asema watanzajia sasa kuachana na nguo za mitumba

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema safari ya Watanzania kuachana na nguo za mitumba imewadia kutokana na uwepo wa viwanda vya kutengeneza nguo nchini.

Pia amesema uwepo wa viwanda hivyo utasaidia wakulima wa pamba kupata soko la uhakika hivyo amewataka walime pamba ya kutosha ili viwanda vipate malighafi.

Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo   Jumamosi, Julai 15, 2017 wakati alipotembelea kiwanda cha nyuzi cha Namera kilichoko Gongo la Mboto na kiwanda cha nguo cha Nida kilichopo Ubungo Dar Es Salaam.

Alisema viwanda vya kutengeneza nguo nchini ni ushahidi tosha kwamba nchi iko njiani kuondokana na matumizi ya nguo za mitumba kwa kuwa nguo nyingi zitakuwa zinatengenezwa nchini, hivyo kupatikana kwa bei nafuu.

Alisema kwa sasa wanunuzi wa pamba hawana sababu ya kwenda kuuza nje ya nchi na badala yake wauze katika viwanda vya ndani ili vizalishe nguo za kutosha zitakazouzwa nchini kwa gharama nafuu.

“Pamba yote inaweza kuchakatwa nchini, hivyo hakuna haja ya kuiuza nje ya nchi. Natoa wito kwa wakulima wetu wa pamba walime mazao ya kutosha kwa sababu soko la uhakika ipo na hii ndio safari ya mwisho ya mitumba.”

Awali Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha saruji cha Lake kinachozalisha saruji ya nyati ambapo aliwapongeza wawekezaji wote nchini kwa kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. John Magufuli za kuifanya Tanzania kuwa ya uchumi wa viwanda.

Katika kiwanda hicho ambacho kinazalisha tani 700,000 kwa mwaka kimeajiri watu 2000 na kinalipa kodi ya  sh. bilioni 81.312 kwa mwaka, Waziri Mkuu aliwataka watumishi wake wawe waaminifu, wafanye kazi kwa weledi na wawe waadilifu.

Pia Waziti Mkuu alitoa wito kwa wamiliki wa viwanda vyote nchini kuhakikisha wanatoa kipaumbele cha ajira kwa wananchi waishio katika maeneo ya karibu na viwanda sambamba na kulipa kodi kwa wakati na kwa viwango sahihi.

MWANAHESABU MSOMI RAIA WA IRAN AMEFARKKI UKO NCHINI MAREKANI.

Maryam Mirzakhani, mwanamke wa kwanza kushinda tuzo la hesabu la Fields Medal amefariki nchini Marekani.

Professor Mirzakhan mwenye umri wa miaka 40 ambaye ni professor katika chuo cha Stanford, alikuwa akiugua ugonjwa wa Saratani ya matiti ambayo ilisambaa hadi kwa mifupa yake.

Alipewa jina mshindi wa Nobel ya hesabu. Tuzo la Fields Medal hutolewa baada ya kila miaka minne kwa kati wa wasomi wa hesabu wawili na wanne walio chini ya miaka 40

TAARIFA KWA UMA KUTOKA IDALA YA UHAMIAJI TANZANIA

Idara ya Uhamiaji inapenda kuwakumbusha Waajiri, Wakurugenzi wa Makampuni, Taasisi mbalimbali na Wageni wote kuhakikisha wamehakiki vibali vyao kupitia Mfumo wa Uhakiki ambao unapatikana kupitia Tovuti ya Idara ya www.immigration.go.tz kabla ya zoezi la uhakiki kuisha tarehe 19/07/2017.

Kwa wale ambao kumbukumbu za vibali vyao hazitaonekana katika mfumo wa uhakiki au kuwa na tatizo lolote wanashauriwa kuripoti katika Ofisi za Uhamiaji za Mikoa au kwa Mamlaka husika ndani ya muda uliotolewa.

Baada ya kuisha kwa muda uliotolewa, Idara itafanya ukaguzi nchi nzima na kuwachukulia hatua za kisheria Wageni binafsi, Waajiri, Wakurugenzi wa Makampuni na Taasisi mbalimbali ambazo wageni wao watabainika kuwa na vibali vya kughushi au vilivyopatikana nje ya utaratibu wa utoaji vibali.

Idara ya Uhamiaji ilitoa muda wa siku 90 kwa wale wote wenye vibali vya ukaazi kuhakiki vibali vyao; tangu tarehe ya kuzindua mfumo huo tarehe 19 Aprili, 2017.

Imetolewa na;

KITENGO CHA UHUSIANO,

MAKAO MAKUU, IDARA YA UHAMIAJI

RAIS KAGAME AJITABIRIA USHINDI WA NGUVU RWANDA

Rais wa Rwanda Paul Kagame tayari anadai kuwa mshindi katika uchaguzi ujao wa Rais utakaofanyika tarahe nne mwezi ujao.

Kagame amewaambia wafuasi wake katika mkutano wa kwanza wa kuanza rasmi kwa kampeni nchini humo kuwa matokeo ya uchaguzi tayari yalijulikana mnamo mwaka 2015 wakati Wanyarwanda waliposhiriki katika kura ya maoni ili bunge kuifanyia katiba mageuzi ya kumruhusu kugombea muhula mwingine.

Kagame amesema wapinzani wake hawawezi kubadilisha mapenzi ya wananchi kuwa yeye ndiye chaguo lao.

Paul Kagame licha ya kuwa anasifiwa kwa kuleta uthabiti katika taifa hilo la takriban watu milioni 12, anashutumiwa na mashirika ya kutetea haki za binadamu kwa kutumia mkono wa chuma kuliongoza taifa na kuwakandamiza wapinzani

Monday, May 15, 2017

Jinsi ya kuzuia na kuondoa chunusi

Wapo watu ambao wanasumbuliwa na tatizo sugu la chunusi, madoa doa na kuharibika kwa ngozi. Ingawa chunusi hizi mara nyingi hutikea usoni, wakati mwingine hutokea pia katika maeneo tofauti ya mwili. Kwa bahati mbaya baadhi ya waathirika wa chunusi wamejikuta wakitumia madawa mengi bila matibabu, hata mara nyingine kuharibu kabisa ngozi zao. Habari njema ni kwamba, imegundulika kwamba matatizo mengi ya ngozi yanayotokea usoni, hasa chunusi ni kwa sababu ya aleji (mzio) ya vyakula tunavyokula, au matatizo mengine yatokanayo na vyakula vya protini. Kwa bahati mbaya, madaktari wengi wa aleji hawawezi kugundua kama chunusi ulizo nazo ni aleji kwa sababu wanafanya allergy test kwenye ngozi, wakati aleji yenyewe iko ndani tena kwenye kiungo specific na yanayoonekana nje ni madhara tu Vyakula mabvyo vimetajwa kuwa huweza kusababisha allergy ni; - Maziwa - nyama - mayai - samaki - kuku - wadudu wanaoliwa kama senene, kumbikumbi nk Hata hivyo sio rahisi kwa mtu mmoja kuwa na allergy ya hivyo vitu hapo juu vyote, na hivyo haimaanishi kama una hilo tatizo basi ndio mwisho wako wa kupata animal protein hapana, ingawa unaweza kuwa na allergy ya kimoja au baadhi ya hivyo. Je, utagunduaje kama chunusi ulizo nazo zinasababishwa na allergy ya kimoja au baadhi ya vitu nilivyotaja hapo juu? Kumbuka, unaweza kutembelea hospitali zote wakafanya allergy tests zote na wasione tatizo, lakini allergy bado iko pale pale. Kwa maana hiyo, namna pekee ni kwa wewe mwenyewe kujifanyia test kama ifuatavyo; 1. Acha kabisa kutumia vyakula vyote vilivyotajwa hapo juu kwa wiki 3. Ina maana kwa wiki hizo 3, utakuwa vegetarian..lol 2. Kama hautaona mabadiliko yeyote, then utagundua kuwa tatizo lako sio allergy hivyo endelea na maisha kama kawaida, huku ukitafuta matibabu mengine. 3. Kama utaona mabadiliko ya kupungua au kuisha kwa tatizo, then mshukuru Mungu wako, maana tatizo lako linaelekea kupata ufumbuzi. Cha kufanya hakikisha tatizo limeisha kabisa ndani ya hizo wiki tatu, au ukiona limepungua halijaisha, then subiri hadi liishe then nenda kwenye step 4 hapo chini... 4. Tatizo likiisha, anza kurudisha kimoja kimoja, ukianza na mayai. Kula mayai 1-2 kila siku kwa siku 7-10 halafu jiangalie kama tatizo lipo. Kama limerudi, acha mara moja kutumia mayai, na subiri hadi liishe kisha ndipo uende step 5 hapa chini 5. Tumia maziwa (kumbuka hii ni siku 10 tangu uanze kutumia mayai). Unaweza kuendelea kutumia mayai (kama hayakuleta tatizo katika step 4), kwa rate ya kawaida uliyokuwa umezoea zamani. Kunywa takribani 200ml hadi 500ml kwa siku kwa siku kumi. Hapa naongelea maziwa ya ng'ombe. Kama unatumia maziwa ya mnyama mwingine, then nayo yawe tested katika step tofauti. 6. Endelea na vyakula vingine vilivyobaki, ukirudisha kimoja kimoja kila baada ya siku kumi, hadi utakapogundua ni kipi kati ya hivyo hapo juu kinachokusababishia tatizo NB; 1. Nyama ya ng'ombe, mbuzi, nguruwe nk ziwe tested tofauti. Nina rafiki yangu anaathiriwa na nyama ya ng'ombe tu sio kitimoto wala mbuzi! 2. Kwa akina dada/mama, tofauti na chakula pia tatizo linaweza kuhusiana na proteins zilizomo kwenye semen za mwanaume/wanaume, na bahati mbaya sana ni kwamba unaweza kuathiriwa na semen ya mwanaume mmoja na sio mwingine! Kivumbi kitakuwa pale unapoathiriwa na semen za mumeo, mbaye kumwambia mtumie condom sio rahisi... Kama tatizo ni hili, hapa inabidi mpime ama kukubali kuishi nalo, au uwe unatumia anti-ellergens kila mnapokutana, lambo ambalo hakuna Dr yeyote duniani atakushauri ufanye. Kama hujaelewa hiyo regime hapo juu, unaweza ukauliza na kupata ufafanuzi mzuri zaidi... 



..Kwa maelezo zaidi piga 0715791042 au 0652943435